Featured

Jipatie nakala ya kitabu chako sasa

Je unayajua mambo yanayokunyima uhuru wako? Hapa nimekuandalia kitabu chenye mambo sita unayotakiwa kuyajua ili uwe huru.
kitabu kimetumia mifano mbalimbali itakayokufanya uelewe zaidi kuhusu vifungo hivyo na jinsi ya kuviepuka.
Kwenye sehemu ya kwanza utajifunza kwa undani mambo manne yanayokufanya uwe kifungoni na jinsi ya kuondoka kwenye vifungo hivyo.
Sehemu ya pili utajifunza maana ya mafanikio.
Sehemu ya tatu utajifunza matendo mema yalivyo na nguvu ya kuwabadilisha wengine.
Sehemu ya nne utajifunza na kuijua nguvu iliyopo pale unapowasikia wengine.
Sehemu ya tano utajifunza zaidi kile kitakachokufanya uwe na maendeleo endelevu.
Sehemu ya sita utajifunza nguvu iliyopo kwenye kumaliza Jambo lolote ulilolianzisha.
Haya ndiyo mambo sita utakayoyapata kwenye kitabu hiki cha UHURU WAKO NI HAKI YAKO YA KUZALIWA.
Kitabu hiki kiko kwenye nakala tete, na utakipata kwa sh 5,000. Tuma pesa kwenda namba 0755034751.
Jina Emanuel mcharo.
Ukishatuma pesa yako tuma email yako pia.
Karibu sana.
Featured

Jipatie kitabu kizuri cha Haufanani nao

Je unajua kitu, kinachokuzuia wewe usifanikiwe? Kinachokuzuia wewe ni tabia yako ya kutaka kufanana na wengine.

Kule kutaka kufanana na wengine, kunazalisha wivu ndani yako. Na pale wivu huo unapokuwa ndani yako, utataka uwaangushe wengine ili uwe juu .

Wewe hutakiwi kujifananisha, na yeyote yule. Unatakiwa kujijua wewe ni Nani, na haufanani na yeyote kwa sura, umri, na hata alama za vidole vyako .

Utawashangaza watu Kama utataka kufanana na mti. Maana kule kutaka kufanana na mti kutaketa wivu ndani yako, kwanini huna rangi ya kijani?

Hapa kuna kitabu, kitakachoenda kukutambulisha, wewe ni wa kipekee kabisa, na hutakiwi kujifananisha na chochote kiwe ndege, dhahabu na hata watu wengine.
Kujifananisha na wengine ni kujitafutia mateso.

Mambo tisa utakayoyapata kwenye kitabu.

1 Ukiwa na malengo ya kufanikiwa kwenye Jambo lolote lile, hakikisha unakuwa na tabia sahihi. Tabia ndiyo itakayovuta watu sahahi kuja kwako.

2 Ulivyo ndivyo ulivyochagua,ukiwa masikini, tajiri unahusika . Utajifunza jinsi ya kujiandaa ili upate yale matokeo unauoyataka.

3 Kinachokurudisha nyuma ni maarifa kidogo uliyonayo.Utajifunza namna ya kukuza maarifa hayo ili yasiwe tena kikwazo kwako.

4 Umejichelewe kwenye maendeleo yako kwa kutaka kukamilisha kila kitu ndiyo uanze biashara yako, ujenzi wako.

5 Tabia mbaya inayokuponza na kukurudisha nyuma ni kuairisha mambo yako.

6 Utajifunza jinsi majaribu yanavyo mtaji wa kupanda viwango.

7 Unaweza kujua jinsi mafanikio kidogo anayopata mtu yanavyokuwa kikwazo kwake kukua zaidi .

8Utajua mshahara wako jinsi unavyoweza kupoteza kuzifikia Ndoto zako.

9 Utajifunza kufikiri kunavyoweza kukuondoa kwenye utumwa wa kutawaliwa na wengine.

Kwa kupata kitabu hiki, utaweza kuyapata mambo haya tisa kwa kina pamoja na mifano mbalimbali. Kimekupa hatua za kuchukua ili ufanikiwe kwenye safari yako.

Kitabu hiki unakipata popote ulipo kwa nakala tete (soft copy.) Kwa sh 10,000.

Kukipata tuma pesa kwenda namba 0755034751. Jina Emanuel mcharo.
Ukishatuma pesa yako tuma pia email yako .
Asante na karibu sana.

KILA JAMBO KWA WAKATI WAKE:


Kila unapopanda daraja la juu kwenye maisha yako, waheshimu wale walio kwenye daraja la chini. Maana uliyo juu leo tambua kuna watu waliamua kukubeba kwenye mabega yao.

Leo unaweza kuona mbele, kwa kuwa uko kwenye mabega ya watu walioamua ukanyage mabega yao. Waheshimu sana watu hao maana wakikususa, lazima utajikuta chini na huo ndiyo utakuwa mwisho wako wa kuangalia mbele kwa kutumia mabega yao.

Siku zote awali ni awali tu hata kama ulipata kidogo bado ndiyo kinayobakia msingi wako. Mwanafunzi wa chuo anaweza kumdharau yule mwalimu aliyemfundisha chekechea. Lakini kiuhalisia anabakia yule mwalimu wa chekechea ndiye aliyemfungulia njia yeye kuweza kukutana na profesa huko kwenye elimu yake ya juu.

Jiulize kama huyo aliyekuonyesha njia awali, angekujengea njia mbovu leo huko juu ungefika?

Lakini hilo la wewe kuwa na elimu kubwa kuliko mwalimu wako wa awali siyo kosa. Maana kulingana na viwango vya maisha ndiyo huamua, pale unapotaka cha juu lazima ukubali kutapoteza kile kilichoko chini yako.

Pale unapoondoka kwenye daraja la chini na kwenda juu, lazima kuna watu utawaacha ili usonge mbele. Na unapoamua kusonga mbele huna haja ya kugombana na mtu au kumdharau yeyote. Ni safari ya muda tu, mnaweza kutoka wote kijijini kwa kutembea kwa miguu. Lakini mkifika kituo cha usafiri kila mtu huchagua usafiri wake.

Naamini umenunua viatu ili vikusitiri miguu yako.
Pamoja na nia yako ya kutaka viatu hivyo vikusitiri, ukifika sehemu yenye matope inakubidi uvivue na kuvibeba.
Unajikuta ile nia yako ya kusitiriwa na viatu inageuka wewe kuvisitiri viatu hivyo.

Kuna kuwa hakuna namna nyingine ni kupambana na hali yako. Unaanza kujiuliza maswali, je niingie na viatu hivi kwenye tope? Au niingie mimi peku nikitoka salama nivirudie viatu vyangu na kuendelea na safari.

Kile utakachokiamua ndiyo kitaamua safari yako iweje.ukiamua kuzamisha viatu kwenye tope ujue hapo ni mwisho wa kuendelea navyo kwenye safari yako.

Uamuzi wote uko juu yako.
Na safari hii ya viatu haina tofauti na safari tuliyonayo kwenye maisha yetu ya kila siku.

Kuna watu watakuwa na wewe kwenye hali fulani, lakini hawa ukifika kwenye matatizo fulani hawatakufaa tena. Utaingia mwenyewe kwenye matatizo yako huku wakitaka wewe uwasaidie.

Hivyo Unatakiwa kujua baadhi ya marafiki, urafiki wao ni kama wa viatu. Pale njia ikiwa nzuri viatu vyako viko na wewe, lakini hali ikibadilika ndiyo mwisho wa urafiki wenu.

Maana Kama utalazimisha viatu vyako uingie navyo kwenye tope basi ujue vitanasa au vitachanika na kuharibika kabisa. Ukiwa na busara lazima uvivue na uvibebe , sasa vimekuwa mzigo juu yako.

Na hili ndiyo somo tunalotakiwa kujifunza, kwamba siyo kila rafiki, utakayekutana naye ataweza kukuvusha kwenye kila changamoto.

Kuna kipindi yule uliyemtegemea atageuka kiatu na inakupasa kumvua na kumweka pembeni ili maisha yaendelee.

Siyo vibaya wewe kuwaweka pembeni baadhi ya marafiki zako ambao wanageuka mzigo. Uking’ang’ana nao utakwama na kuchafuka na huo utakuwa mwisho wa safari yako.

Unapoifikia changamoto kubwa, pambana na hali yako, na tafuta marafiki wenye uwezo wa kuimudi hiyo changamoto unayoipitia. Tafuta wale unaweza kuvuka nao ng’ambo. Na waheshimu wale uliowaacha wakiendelea na maisha yao bila wewe kuwatusi au kuwadharau.

MAISHA NI NINI?

Maisha ni kuumba. Unaweza kuipata maana halisi ya maisha yako ikiwa utaamua kuitengeneza maana hiyo. Maisha ni kama shairi linalosubiria kutungwa.

Maisha ni wimbo unaotakiwa uimbwe, ni mziki unaotakiwa uchezwe. Maisha kama maisha hayana maana, maisha ni fursa ya kutengeneza maana.

Maana hiyo haitakuwa kitu kinachotakiwa kuvumbuliwa. Bali maisha ni kitu kinachotakiwa kiundwe. Maana ya maisha unaweza kuipata kwa kutengeneza aina ya maisha yale unayoyahitaji.

Maisha siyo kitu unachoweza kuzunguka nyumba na kukutana nacho. Au useme ni kitu kilichopotea ukikitafuta kidogo utakipata. Maisha siyo madini, useme ukiyachimba utayakuta. Maisha halisi ni kama mashairi yanayotakiwa yatungwe.

Maana ya maisha ni kucheza mziki na siyo kukutana nao. Huwezi kukutana na mziki, na maana ya mziki ni ucheze.

Maana utakayoipata kwenye maisha yako ile tu uliyoitengeneza, na hilo ndiyo jambo la muhimu kukumbuka.

Wengi wetu tumekwama kwa kuwa tunafikiri maisha ni kitu kinachopaswa kuvumbuliwa, kama kitu hicho kilikuwepo tayari.

Watu wanafikiri maisha ni kama kupasua mwamba na kuyakuta madini. Maisha hayana maana hiyo kwamba paa kitu kimetokea kiko hapa. Utawakuta vijana wa siku hizi wakisema one day yes. Wakifikiri ipo siku maisha yenyewe yatatokea kama dodo chini ya mwembe.

Kumbuka hakuna maana nyingine ya maisha zaidi ya ile uliyoitengeneza. Ukiona Kuna maana yoyote kwenye maisha yako ni sababu wewe unahusika kuitengeneza.

Mungu siyo kitu zaidi ya mwumbaji. Na yeyote anayetaka maana ya maisha anatakiwa ayaumbe.

Maisha siyo kitu kilicholala sehemu fulani. Siyo kitu kinachohitaji kuvumbuliwa. Kama ingekua ni kitu kinachohitaji kuvumbuliwa basi mtu mmoja angetosha kuvumbua. Na kusingekuwepo na haja ya kumta kila mtu avumbue. Kwa kuwa maisha ni kuumba basi kila mtu lazima aumbe maisha yake anayoyataka. Na kule kuumba maisha yako ndiko kunakoyapa maisha maana.

Changamoto zile tunazopitia,ndiyo zenye uwezo wa kutufanya tukue.

Kile kinachoendelea kukuzunguka kwenye maisha yako kisiwe kikwazo kwako. Pale unapoenda baharini, unaweza kuyaona mawimbi maelfu kwa maelfu.

Lakini kwenye vilindi vya bahari hiyo kunakuwa na utulivu na ukimya mkubwa. Mawimbi yote huonekana kwenye uso wa bahari tu.

Zama ndani yako kwa tahajudi na sala, maana mahangaiko na misuguano ni kwa nje tu, ndani yetu kunao ushindi mkubwa ambao hauwezi kufikiwa na yale yanayotuzunguka.

Kama ilivyo kwenye vilindi vya bahari visivyoweza kufikiwa na mawimbi basi ndani yetu hakuwezi kufikiwa na kile kinachotusumbua kwa nje. Iwe umasikini, ugonjwa nk. Tuyachukulie maisha yetu Kama majaribio ya kisayansi.

Wanasayansi wako imara sana ndani yao. Pale wanaposhindwa jaribio la kiutafiti, hawakati tamaa bali hutumia kushindwa huko kama kituo cha kuwaongoza kwenda kwenye mafanikio.

Jiulize ni majaribio mangapi wameyafanya na kuanguka kwenye kupata dawa ya kuutibu ukimwi? Ni majaribio mangapi yamefanyika kwenye ugonjwa wa uviko 19.

Kumbuka wanasayansi wanatumia kila anguko kama kituo muhimu kwao kinachowasaidia kusonga mbele.

Sisi pia tunatakiwa kuwa kama wanasayansi,kutumia kila anguko tunalopata kama sehemu ya kusonga mbele. Na tusiruhusu kile kinachotuzunguka kwa sasa kuwa kikwazo,bali tukitumie kama kituo cha kuendelea mbele.

USHINDI NI LAZIMA KWAKO USIKATE TAMAA:

Inawezekana uko kwenye hali ngumu, na unafikiri hakuna tena tumaini. Ni kweli inaweza kufikiriwa hivyo. Lakini pale unapotambua kuwa Unatakiwa uwe kwenye hali nzuri, unapata nguvu kubwa ya kupambana.

Tuchukulie umeteguka mguu, na akatokea mtu anakuambia kimbia. Utaanza kujitetea jinsi gani huwezi kukimbia,na hata watu wanaweza kukutetea kulingana na hali wanayokuonanayo.

Lakini hapo hapo katikati ya mabishano ya kwanini huwezi kukimbia, akatokea mtu mwenye bunduki na anataka akue utashangaza watu kwa kasi utakayokimbia. Unapata nguvu kubwa pale unapojua uhai ni muhimu kuliko maumivu ya kuteguka.

Kule kujua Unatakiwa kuwa hai kunakupa sababu ya kuyashinda maumivu. Ni kweli ilionekana huwezi kukimbia, lakini hilo haliwezi kukufanya umsubiria yule mwenye bunduki akufikie ulikuwa umekata tamaa ya kukimbia.

Kwa vyovyote vile utafanya jitihada za kujiokoa. Kule kuhisi kukosa matumaini ni njia iliyotengenezwa ili ujihisi wewe ni mnyonge lakini sivyo ulivyo hata kidogo. Unakuta jengo la ghorofa za juu linawaka moto,na watu wanaokoa maisha yao kwa kuruka. Miongoni mwa watu utakaowaona wakiruka kutoka juu ni wale waliofikiriwa hawataweza kuruka. Watu huruka na sababu ni kutafuta ushindi.

Uwe na matumaini ya ushindi kuliko kung’ang’ania kukata tamaa. Unapokuwa na matumaini ya kuwa hai ndipo unapopata fursa ya kushinda vizuizi vilivyopo mbele yako. Hakuna hali mbaya kama utakuwa na uwezo wa kuendelea kujaribu. Na uamini chochote kinaweza kutokea huko mbele ya safari.

Timu ya mpira inaweza kufungwa magoli 3 mapema. Lakini wachezaji huendelea kupambana hadi dakika ya mwisho. Utashangaa kuiona timu iliyokuwa imefungwa goli 3 ikiibuka na ushindi wa 4-3 kwenye dakika za mwisho.

Mashabiki wa timu iliyotangulia kufungwa walivyoona dakika zilizobakia walikata tamaa ya timu yao kushinda. Wengi walianza kuondoka uwanjani, wale wa majumbani walibadilisha channel za runinga zao, wale wa redio walizima redio zao. Lakini katika kipindi hicho kidogo timu yao ilibadilika na kuleta matokeo yasiyotarajiwa ya kushinda goli 4-3. Chochote unachopitia kama uko hai amini ushindi upo. Siri ya washindi ni kubakia kwenye mchezo hadi dakika ya mwisho.

Mwandishi wa makala ni Emanuel mcharo. Barua pepe mcharoima@gmail.com

KUANGUKA SIYO MWISHO WA SAFARI:

Karibu rafiki  yangu kwenye makala yetu ya leo.

Leo tunaenda kuangalia kwanini tunapitia kwenye nyakati ngumu.Nyakati ngumu zimekuwa ndiyo mwalimu mkuu kwetu.

Pale unapopitia nyakati ngumu zinakufanya ufanye maandalizi ya  kubeba majukumu yako yatakayokuwezesha kufikia mafanikio yako

Watu huwa hawajali sana kile unachokisema,bali hujali kile unachokifanya.Hakuna mtu anayetaka kuwa masikini,hakuna anayetaka kuteseka.

Kila mmoja wetu anayo nia ya dhati ya kupambana ili kuyafikia malengo yake. Hivyo inapotokea ukakwama jua ni mojawapo ya mambo yaliyopo kwenye safari yako.

Kumbuka mshale unaweza kufyatuka pale unapovutwa kwenda nyuma.Pale unapoona maisha yakikurudisha nyuma na kupitia magumu jua yanakwenda kukupatia kitu kikubwa huko mbele.Hivyo ongeza nguvu na endelea kupambana.

Jisamehe kwa maamuzi mabaya uliyoyafanya.Jisamehe kwa makosa yako uliyoyafanya.Jua kinachotakiwa ni wewe kusonga mbele huku ukiwa umeshajua nini kilikufanya ukaanguka mwanzo.

Unapaswa kuachana na vitu vyote ambavyo huwezi kuvidhibiti.Kama umepata hasara kubaliana nayo.Hivyo jiimarishe ondoa wasiwasi,futa aibu.Jijali na uwajali wale wote walio na umuhimu kwako.

Pambana kuifikia ndoto yako,na hakikisha unajipenda kwanza wewe, vinginevyo hakuna anayeweza kufanya hivyo kwa niaba yako.

Pale utakapofanya vitu vyako vizuri utawavutia watu ambao watataka kuwa na wewe.Na pale utakapozungukwa na watu sahihi ndipo utakapoanza kuyaona mafanikio yako.

Kumbuka Ndoto zako zitaendendelea kutimia kwa wewe kuendelea kukuza biashara yako,na kuanzisha biashara nyingine mpya.

Hivyo endelea na mapambano fanya kazi kwa bidii na maarifa.Weka nidhamu kwenye kazi yako na utakapogundua pochi yako utaiona faida ya uwekezaji wako.

Maisha mazuri ni fursa kwa wale wote waliotayari kuyapambania,na siyo wale wanaokaa na kuwaangalia wengine . Usiogope ukaipoteza fursa ya wewe kuwa na maisha mazuri ya Ndoto yako.

Usiache kujaribu maana kila mafanikio huanza na wazo la kutaka kujaribu.ujinga na woga huharibu fursa nyingi.hujachelewa anza leo kufanya kile unachokitaka

Mwandishi wa makala hii ni Emanuel mcharo.wasiliana naye kwa barua pepe mcharoima@gmail.com.

WEWE NI KIONGOZI WA MAISHA YAKO:

Karibu  sana rafiki yangu kwenye blog yako ya mshindi.

Kamwe kwenye maisha yako usisahau wewe ni baharia wa meli yako.Jambo la kuwa kiongozi wa Maisha yako ndilo linalokufanya uhitaji kujifunza kila siku ili uweze kukua zaidi.

Baharia kipindi anajifunza  kuiendesha meli lazima ajifunze kuyazoea mawimbi ya maji.Azoee hali mbalimbali za mabadiliko ya hali ya hewa.Awe na tahadhari kwa matukio yanayoweza kutokea bila ya kutarajia.

Kama ilivyo kwa maisha ya baharia,ndivyo ilivyo pia kwenye maisha yetu.Utakutana na vikwazo mbalimbali kwenye safari ya maisha yako.Yawezekana ukawa na mipango mingi mizuri lakini ikaharibika,na viko vitu vingi vinavyoweza kutokea nje ya udhibiti wako.

Kwa vyovyote vile ,matarajio aliyonayo baharia ni kuifikisha meli yake bandarini kwa usalama.Iwe anaogopa mawimbi au la inamlazimu kupambana kuhakikisha anatimiza jukumu lake kwa ufasaha.

Nini kinamfanya baharia kuwa imara,zidi ya mawimbi makubwa ambayo muda wote huiiyumbisha meli?jibu ni moja tu ni mbinu mbalimbali alizo nazo za kukabiliana na hali inayojitokeza.Ukubwa wa mawimbi haumfanyi baharia kuacha kuendelea na safari yake.

Ni kweli kabisa wakati mwingine anaweza kuogopa kufa,lakini kwa kuwa anaijua kazi yake,anaamua kupambana.Anajua  kukimbia kuiongoza meli yake zidi ya mawimbi hayo hakutasaidia chochote.Anafahamu bila kupambana na kuielekeza meli yake vyema chochote kinaweza kutokea na kuizamisha meli yake haraka.Hivyo anajua vyoyote itakavyokuwa lazima apambane zidi ya dhoruba yoyote.

Vivyo hivyo kwenye maisha yetu ya kila siku,Kuna kupitia dhoruba mbalimbali.Ni muhimu kujifunza mbinu za kukabiliana na chochote kinachoenda kutokea,vinginevyo dhoruba hizo zitatushinda na tutakuwa tumeanguka kabisa.

Baharia mwoga au yule anayejiona anaweza kuwa na bahati mbaya yeye huwa anasubiria mpaka kipindi bahari inapokuwa na utulivu,ndipo anapoweza kwenda na inapotokea dhoruba isiyotarajiwa hushindwa.

Baharia imara huwa hamlaumu yeyote bali yeye binafsi,na hujifunza kupitia makosa yake,na ikitokea kipindi kingine cha dhoruba yeye huhakikisha anashinda.Anajua kilichomkwamisha hapo awali ni upungufu wa mbinu alizokuwa nazo.Hivyo huamua kwenda kwa mabaharia wengine na kujishusha ili kujifunza mbinu wanazotumia wenzake .Anapojua vyema hurudi na kuendesha meli yake mwenyewe.

Haya ninayokueleza hapa usijisahau ukafikiria nilikuwa nakuhadithia habari za mabaharia wa meli au maboti.Hapana,hapa ninachokuelezea hapa ni habari ya wewe na maisha yako.

Na Kama hujui nini cha kufanya ni muhimu kuwatafuta watu watakaokufundisha jinsi ya kufanya hadi na wewe uweze kufanya mwenyewe.Kwa vyovyote vile fanya vile vitu vitakavyokufanya kuwa baharia kwa meli yako mwenyewe.

Unayaangalia maisha yako na unajiona unaweza kuwa mshindi.Lakini lazima uwe Kama yule baharia imara ili uweze kuwa mshindi.Haijalishi ni kwa kiasi gani unaihofia safari yako,bali kinachotakiwa ni kwa namna gani unaweza kupambana ili kuishinda hofu yako na kusonga mbele.Fanya miugiza itokee,haijalishi ni dhoruba gani imekupata kwenye maisha yako.Wewe jiandae na uwe na mbinu mbalimbali za kuibuka mshindi.

Mwandishi wa makala hii ni Emanuel mcharo barua pepe ni mcharoima@gmail.com.

Design a site like this with WordPress.com
Get started